Idadi ya watuhumiwa wa tukio la kulipua bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, yaongezeka

Idadi ya watuhumiwa wa tukio la kulipua bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya OLASITI mkoani ARUSHA Jumapili iliyopita imefikia watu 12.

Watuhumiwa hao wametajwa na Jeshi la Polisi kuwa ni VICTOR KALISTI na JOSEPH LOMAYANI, ambao wote ni waendesha bodaboda wakazi wa KWA MROMBO mkoani ARUSHA.

Kamanda wa Polisi mkoa wa ARUSHA, Kamishna Msaidizi wa polisi LIBERATUS SABAS amewataja watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kuwa ni GEORGE SILAYO, mfanyabishara na mkazi wa OLASITI; MOHAMED SAID, mkazi wa ILALA mkoani DAR ES SALAAM, ambaye ametajwa kuwa ni mwenyeji wa watuhumiwa raia wa Uarabuni.
Wengine wanaoshikiliwa ni SAIDI ABDALLAH SAID, raia wa Falme za Kiarabu; ABDULAZIZ MUBARAK, mkazi wa SAUDI ARABIA; JASSINI MBARAK, mkazi wa Bondeni ARUSHA; FOUD AHMED, raia wa Falme za Kiarabu na SAID MOHSEN, mkazi wa NAJRAN- Falme za Kiarabu.

Jeshi la Polisi nchini kupitia Mkuu wake, Inspekta Jenerali, SAID MWEMA limetangaza donge nono la shilingi milioni 50
kwa mtu yeyote atakayefanikisha kufichua mtandao wa kigaidi nchini.
chanzo  CG FM RADIO

SPORTS BOX

Phasellus facilisis convallis metus, ut imperdiet augue auctor nec. Duis at velit id augue lobortis porta. Sed varius, enim accumsan aliquam tincidunt, tortor urna vulputate quam, eget finibus urna est in augue.

No comments: