LINEX AKATAA KUFUNGA NDOA KWA FASHENI


.
                          Sunday Mangu ‘Linex’ akiwa na mchumba wake Suvi Rikka.

KUTOKANA na ndoa za mastaa wengi kuvunjika, msanii wa muziki wa kizazi kipya, Sunday Mangu ‘Linex’ amefunguka kuwa japokuwa ana mchumba hayupo tayari kuoa kwa fasheni kwa kumuiga mtu f’lani 
 kwani anaogopa kuharibu dira nzima ya maisha yake.

Akichezesha taya na paparazi wetu juzikati, Linex alisema kwa sasa yeye na mchumba wake Mzungu aitwaye Suvi Rikka bado wanasomana na kila mmoja akisharidhika na tabia ya mwenzake ndipo suala la ndoa litafuata.
 
“Mimi sitaki kuoa kwa fasheni eti kwa kumfuata mtu f’lani na sitaki kufunga ndoa leo halafu kesho imevunjika, nataka mimi na mke wangu tuishi milele,” alisema Linex.

SPORTS BOX

Phasellus facilisis convallis metus, ut imperdiet augue auctor nec. Duis at velit id augue lobortis porta. Sed varius, enim accumsan aliquam tincidunt, tortor urna vulputate quam, eget finibus urna est in augue.

No comments: