Lulu akataa kuongea na vyombo vya habari


Mwigizaji maarurfu wa bongomovies Elizabeth Michael alimaarufu kama Lulu,  amesema bado hajawa teyari  kuzungumza na vyombo vya habari vinavyotafuta kufanya naye interview baada ya mrembo huyu kuachiliwa kwa dhamana kuhusu kesi inayomkabili kuhusiana na kifo cha  marehemu Steven Kanumba ambaye alikuwa mpenzi wake.
Taarifa za kuaminika zilizopatikana toka kwa mmoja wa watu wa karibu sana na Lulu zinasema kuwa, mwanadada huyu atakuwa huru kuzungumza na vyombo vya habari katika siku chache zijazo ila kwa sasa kwani bado anapata mapumziko ya binafsi na pia anajiandaa kutoka na filamu mpya ambayo ndiyo itakuwa kama utambulisho mpya wa mwigizaji Elizabeth Michael baada ya kutoka jela alipokuwa akishikiliwa kwa takribani mwaka mmoja.

SPORTS BOX

Phasellus facilisis convallis metus, ut imperdiet augue auctor nec. Duis at velit id augue lobortis porta. Sed varius, enim accumsan aliquam tincidunt, tortor urna vulputate quam, eget finibus urna est in augue.

No comments: