Kipa wa kikosi cha Marsh Academy amefariki dunia akiwa uwanjani.
Taarifa, zinaeeleza, Sylvetsre Laang maaurufu kama Chura amefariki dunia baada ya kukanyagwa akiwa uwanjani.
“Kweli Chura amefariki baada ya kukanyagwa na fowadi wakati wakiwania mpira. Lakini amefia kwao Mahenge na taarifa zimeletwa Mwanza,” alieleza Thomas aliyedai ni mmoja wa wahusika wa Academy iliyokuwa na marehemu Marsh.
“Alikuwa amekwenda kwao Mahenge kwa mapumziko, huko ndiko matatizo yalipomkuta,” alisisitiza.
TUNAENDELEA KUFUATILIA TAARIFA ZAIDI TUTAKUJULISHA
![]() |
| BAADHI YA WACHEZAJI WA KITUO CHA MARSH ACADEMY |

No comments:
Post a Comment