STAND UNITED YAWANASA KIEMBA NA DILUNGA KWA MKATABA WA MWAKA MOJA

Kiungo mkongwe, Amri Kiemba amejiunga na Stand United ya Shinyanga.


Kiemba pamoja na kiungo wa zamani wa Yanga, Hassan Dilunga wametua Stand United ambayo sasa inadhaminiwa na kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia.

Msemaji wa Stand United, Deokaji Makomba amesema wachezaji hao, kila mmoja amesaini mkataba wa mwaka mmoja.

“Kiemba anatarajia kurejea hapa Shinyanga leo kuungana na wenzake kwa ajili ya kwenda Kahama ambako tutaweka kambi.

“Pia Dilunga suala lake limemalizika naye amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Stand, chama la wana.”

Mara ya mwisho, Kiemba aliichezea Azam FC ambayo alijiunga nayo akitokea Simba.
Amri kiemba
                                             
                                 Hassan Dilunga

SPORTS BOX

Phasellus facilisis convallis metus, ut imperdiet augue auctor nec. Duis at velit id augue lobortis porta. Sed varius, enim accumsan aliquam tincidunt, tortor urna vulputate quam, eget finibus urna est in augue.

No comments: