FIFA yaziachia huru klabu za real madrid na atletico madrid

shirikisho la soka la soka duniani (fifa) limefuta adhabu iliyokuwa inavikabili vilabu vya real madrid na atletico, ambapo kwa sasa ziko huru kwa usajili hadi hapo zitakapo sikilizwa rufani zao na shirikisho hilo.
klabu zote mbili ziliandika katika taarifa zao kuwa fifa imeziachia huru kuendelea na usajili wa wachezaji mara baada ya kufungiwa kufanya hivyo kutokana na kufanya usajili wa watoto, kinyume na utaratibu.
real madrid na atletico zote ziliwasilisha rufani zao kwa shirikisho hilo na sasa zitaendelea kuwa huru hadi hapo fifa itakapopitia upya kesi zao na kufanya maamuzi.
adhabu kama hiyo iliikumba klabu ya barcelona mwaka 2014 na kushindwa katika rufaa yao,  kitu kilichopelekea klabu hiyo kusajili wachezaji arda turan na alex vidal ambao imeanza kuwatumia mwezi huu wa january mara baada ya kumaliza kifungo.

SPORTS BOX

Phasellus facilisis convallis metus, ut imperdiet augue auctor nec. Duis at velit id augue lobortis porta. Sed varius, enim accumsan aliquam tincidunt, tortor urna vulputate quam, eget finibus urna est in augue.

No comments: