John Terry kustafu kuihama chelsea baada ya msimu huu kuisha

Nahodha wa Chelsea John Terry anatarajiwa kuihama klabu hiyo mwisho wa msimu huu mara baada ya kupewa taarifa na uongozi kuwa hatoongezewa mkataba mpya kuendelea kuichezea klabu hiyo yenye maskani yake Stamford Bridges.

 Terry aliweka wazi taarifa hiyo mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa kombe la FA walipoishinda klabu ya MK Dons magoli 5-1 na kutinga hatua ya 16 bora,  kuwa baada ya kukaa na uongozi wiki iliyopita aliambiwa kuwa hatopewa mkataba mpya mezani.


 Kama ataondoka klabuni hapo,  John Terry amesisitiza kutojiunga na klabu yeyote ile ya ligi kuu nchini England na kwamba anaumia kuondoka kwa namna hii kwa klabu aliyoihudumia kwa miaka 21 hadi sasa.

 Ingawa taarifa ya klabu baadae ikasema kuwa ni kweli kuwa walimtaarifu John Terry kuwa hatopewa mkataba mpya, lakini kwa kuheshimu huduma ya nahodha wao huyo wapo tayari kwa mazungumzo na lolote linaweza tokea katik miezi kadhaa ijayo.

 Wachambuzi mbalimbali nchini England wameshangazwa na kitendo hiki cha kukosa utiifu kwa klabu ya Chelsea dhidi ya wachezaji wake walioisaidia timu yao kwa maisha yao yote,  Jamie Carragher na wachambuzi wengine wengi wanam-rate John Terry kuwa miongoni mwa mabeki bora zaidi katika historia ya ligi hiyo.

SPORTS BOX

Phasellus facilisis convallis metus, ut imperdiet augue auctor nec. Duis at velit id augue lobortis porta. Sed varius, enim accumsan aliquam tincidunt, tortor urna vulputate quam, eget finibus urna est in augue.

No comments: